Posts

Showing posts with the label MAHUSIANI NA NDOA

Hizi ni njia Tatu zinazoweza Kusaidia Mahusiano yako Kudumu Kwa Muda Mrefu

Image
Mahusiano mengi yamekuwa yakivunjika kwa kushindwa kudumu kwa muda mrefu kutokana na kila mtu kumchoka mwenzake. Unaweza kuwa katika uhusiano kwa muda mrefu na kamwe usichoke kumwona au kutaka zaidi kutoka kwa mpenzi wako. Hizi ni njia tatu zinazoweza kusaidia mahusiano yako kudumu kwa muda mrefu: Geuza mtazamo wa mapenzi Unapaswa kutumia kila nafasi unayoipata kufanya mapenzi kama nafasi ya kumuonyesha kitu kipya mpenzi wake – Mwisho utagundua kitu kutoka kwa mpenzi wako huyo! Jitahidi kusoma na kujifunza njia mpya kwa ajili ya kumfurahisha mpenzi wako hali itakayopelekea kumlinda mpenzi wako asitoke nje ya mahusiano yenu. Watu wengi wamezoea kuwa mwanaume ndio kiongozi wa kila kitu, hali iliyopelekea mpaka wanawake wengi hawezi kumuambia mtu wake kuhusu kufanya ‘tendo’ mpaka mwanaume ndio aanze kusema. Hilo kwenye mapenzi ni kitu ambacho kinapaswa kuwekwa kando ili kuleta furaha kwenye mapenzi yenu. Tafuta ushauri Kuna mbinu nyingi ambazo wapenzi hudhani wanazijua, lakini ni njia moj...

HIZI HAPA NI AINA NNE ZA WANAWAKE WACHEPUKAJI

Image
1.MCHEPUKO LAMI: Huu ni ule ambao hauombi pesa, katulia hana mapepe, uwe naye au usiwe naye maisha yake yanaendelea tu. 2. MCHEPUKO VUMBI: Huu ni ule wa vibomu!! mara ooohhh sina pesa, naomba vocha, sijui simu imekufa, oooh mara nipo saluni nadaiwa elf thelathin, naomba nauli.....n.k! Na hii ndio noma maana njia kuu lazima washtuke mana mchepuko vumbi unachafua na unasumbua full time. 3. MCHEPUKO KOKOTO: Huu ni mkali zaidi ya njia kuu maana kila mara huuliza upo wapi, Uko na nani, why hupokei simu yangu? Kama uko kwako naomba utoke nje tuongee kidogo na leo uwe na mimi tu...Yaani tabu tupu! 4: MCHEPUKO MATOPE: Yaani huu usiombe hata kukutana nao maana wenyewe ndio funga kazi.. Huu bana unajua kuchuna hasa ila pale unapoupa pesa na wenyewe unaenda kuzihonga zote kwa mchepuko wake mwingine yaani hatari tupu.

Mambo ya Msingi Kuyafanya Kabla ya Kuoa/Kuolewa

Image
Ndoa nyingi zinaingia kwenye migogoro kwa sababu ya mambo ya kukurupuka na kufanya haraka bila wahusika kufahamiana vizuri, hebu tuzingatie yafuatayo ili tusiseme 'NINGEJUA NISINGEOA/NISINGEOLEWA' 1. Chanzo cha uhusiano wenu kiwe ni upendo wa dhati 2. Chunguza kwa mwenzio juu ya tabia:nidhamu, adabu, hasira, ulevi na umalaya 3. Mpeane muda wa kutosha kufahamiana 4. Mtembee pamoja maeneo tofautitofauti kama michezoni, bar na out mbalimbali ili muone interest za kila mmoja 5. Muwe wa imani moja. ila kama mmeshibana sana na mwaweza kuvumiliana hata wa imani tofauti ni sawa. 6. Wajue ndugu wa mwenzio ili kupata habari zao zitakazokufahamisha mwenzao pia yukoje 7. Pimeni afya zenu bila aibu. kuna maradhi mengi kama HIV/AIDS na mengine. 8. Kama ni Mkristo au Muislam funga ndoa Kanisani au Msikitini na siyo Bomani. 9.Kwa Wakristo ndoa haina talaka. huu ni mpango wa Mungu. kuachana na kuoa mwingine ni dhambi.