JPM- WATANZANIA OMBEENI AMANI

Rais Magufuli alisema pamoja na Watanzania wote kuungana kuombea amani na utulivu, pia hawana budi kutekeleza kwa vitendo maandiko matakatifu ya Biblia yasemayo “Asiyefanya kazi na asile” kwa kuhakikisha kila mmoja anachapa kazi kwa juhudi na maarifa ili kuharakisha maendeleo ya Taifa.

“Ndugu zangu nawashukuru sana, muendelee kuliombea taifa hili, taifa letu ni la umoja, sisi wote ni Watanzania, tuendelee kumuomba Mola wetu, kudumisha amani yetu, kujenga umoja wetu kwa dini zote, makabila yote na vyama vyote, kwa sababu Mola wetu anatupenda sisi sote,” alisema Rais Magufuli.


Aidha, baada ya kuwasalimu waumini wa Kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato, Rais Magufuli aliendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa jengo jipya la kanisa hilo, ambapo Sh milioni moja zilikusanywa papo kwa hapo.
RAIS John Magufuli ametembelea msikiti na makanisa yaliyopo Chato mjini mkoani Geita na kuendelea kuwasihi Watanzania kuombea amani na utulivu katika nchi, bila kujali tofauti za dini, makabila na kanda wanazotoka.

Rais alitoa ujumbe huo mara baada ya kusali ibada ya Jumapili katika Kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato. Baadaye alitembelea Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Stephano Parokia ya Chato, Kanisa la African Inland Church la Chato na kumalizia katika Msikiti wa Omar Bin-L-Khattab wa Chato.

Comments

Popular posts from this blog

MREMBO GIGY MONEY AFANYA KUFURU NYINGINE

Hamorapa kuhusu Ishu ya kumpigia Alikiba Magoti .