PESA ZA ELIMU BURE ZAANZA KUTAFUNWA

pesa

FEDHA zilizotengwa na Rais John Magufuli kwa ajili ya kugharimia elimu ya bure nchini, zimeanza kutafunwa baada ya kubaini kuwapo kwa udanganyifu unaofanywa na walimu wakuu kwa kuongeza idadi ya wanafunzi hewa ili kupata fedha zaidi.

Kutokana na hali hiyo, wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam na Manispaa ya Arusha, zimebaini udanganyifu huo na kuchukua hatua za awali kwa kusimamisha walimu wakuu wa shule husika na pia kuziagiza mamlaka husika kuwavua uongozi walimu hao.

pesa

Hivi karibuni, Rais Magufuli aliwaagiza wakuu wa wilaya zote, kushughulikia udanganyifu unaofanywa na walimu wakuu wanaotafuna fedha kwa kuweka wanafunzi hewa katika suala la elimu bure baada ya serikali kuanza kutoa elimu bure Januari mwaka huu, ikitenga Sh bilioni 18.7 kila mwezi.

Wanafunzi hewa Kinondoni

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi aliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam kuwa kubainika kwa wanafunzi hao kumekuja baada ya kuagiza mkurugenzi na watendaji kufanya uhakiki shule kwa shule ili kubaini wanafunzi hewa, waliowekwa na walimu wakuu wasiokuwa na uzalendo na kujipatia fedha kinyume cha sheria.

“Hadi kufikia leo (jana) tumebaini wanafunzi hewa 3,462 kutoka shule 68 za msingi na wanafunzi 2,534 kutoka shule 22 za sekondari ambao wameingizwa, ni jambo la kusikitisha fedha za serikali zinapotea kwa sababu ya walimu wakuu wasio waaminifu,” alisema Hapi.

source MTEMBEZI.COM

Comments

Popular posts from this blog

MREMBO GIGY MONEY AFANYA KUFURU NYINGINE

Hamorapa kuhusu Ishu ya kumpigia Alikiba Magoti .