SITTA AREJEA NCHINI KUTOKA UJERUMANI ALIKOENDA KUTIBIWA MIGUU


Spika wa Bunge mstaafu, Samuel Sitta amerejea nchini kutoka Ujerumani alikokwenda kwa ajili ya matibabu ya miguu.

Septemba mwaka huu, Sitta alikwenda nchini humo baada ya kusumbuliwa na tatizo hilo.

samuel-sitta

Mmoja wa wanafamilia wa mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa waziri wa wizara mbalimbali serikalini, alimwambia mwandishi wa habari hizi kuwa hali yake inaendelea vizuri.

 Hata hivyo mimi siyo msemaji wa familia,” alisema mtoa habari huyo.

Alipotafutwa mke wa Sitta, Margaret ambaye alirithi ubunge wa Urambo kutoka kwa mumewe, alisema alikuwa benki na asingeweza kuzungumza  na simu.


 

Comments

Popular posts from this blog

Mtoto wa Miaka minne Auawa, Atupwa Kisimani

MOURINHO KUWAPIGA BEI WACHEZAJI 13 MAN UNITED

MWANAFUNZI Anusurika Kifo Baada ya Kukatwa Mapanga na Mwalimu