Posts

Showing posts from March, 2017

Waziri Mkuu Ataka Mkataba Uvunjwe....Ni wa Mkandarasi aliyenyang’anywa pasipoti na Rais Magufuli

Image
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haitavumilia wakandarasi wasio na uwezo na ambao wanapewa kazi lakini wanashindwa kuzimaliza katika muda uliopangwa. Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo, jana (Alhamisi, Machi 30, 2017) wakati akizungumza na watumishi wa Halmamshauri ya Chalinze na wale wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira (CHALIWASA) katika ofisi zao, karibu na daraja la mto Wami, wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani. Alikuwa ameenda kukagua mradi wa upanuzi wa mtambo wa maji Chalinze na ujenzi wa mfumo wa kusafirisha na kusambaza majisafi pamoja na matenki ya kuhifadhia maji ambao umechukua muda mrefu lakini haujakamilika. Awamu ya kwanza ilianza mwaka Septemba mosi 2001 na kukamilika Desemba mosi 2003. Alimuagiza Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge ahakikishe kuwa kazi ya ujenzi wa mradi huo inaimarika na kufikia asilimia 80 la sivyo, wakamilishe taratibu za kukatisha mkataba na kutafuta mkandarasi mwingine. Agizo la Waziri Mkuu linafuatia taarifa aliyopewa kw...

Bajeti ya Kenya ya mwaka 2017/2018 Yasomwa.....Ajira Sekta ya Umma Zasimamishwa

Image
  Bajeti ya Kenya ya mwaka 2017/2018, imesomwa jana kinyume na inavyosomwa kawaida mwezi Juni, kutokana na uchaguzi mkuu utakaofanyika Agosti mwaka huu, huku ikitangaza kusimamisha ajira katika sekta ya umma. Katika bajeti hiyo ya shilingi za Kenya trilioni 2.6 (Takriban shilingi trilioni 52 za Tanzania) Waziri wa Fedha, wa nchi hiyo, Henry Rotich ameondoa kodi kwenye mahindi yanayoagizwa kutoka nje kwa kipindi cha miezi minne ijayo, Aidha kodi imeondolewa kwenye dawa za kuulia wadudu za nchini humo pamoja na magari ya utalii yanayoundwa nchini Kenya. Katika bajeti hiyo ambayo ni ya mwisho kwa serikali ya Jubilee katika muhula wake wa kwanza, serikali imeongeza kodi kwenye kamari hadi 50% kutoka 7.5% ya awali kama njia ya kukomesha uchezaji kamari. Serikali pia imetangaza kusimamisha ajira katika sekta za umma isipokuwa sekta ya elimu kama njia ya kupunguza matumizi. Jumla ya Shilingi bilioni 524.6 za kenya katika bajeti hiyo zitatokana na mikopo kutoka nje na ndani ya nchi. Shili...

Jaji Mkuu Ampa Majukumu Tundu Lissu

Image
Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa   Ibrahim Juma ameutaka uongozi mpya wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kuusoma na kuuelewa mpango mkakati wa miaka mitano wa Mahakama ya Tanzania ili umoja huo uweze kuchangia katika kuutekeleza. Aliyasema hayo jana alipotembelewa na uongozi wa   TLS ulioongozwa na Rais wa chama hicho,    Tundu Lissu. Alisema    ni vema kuusoma Mpango Mkakati huo   kufahamu ni wapi mahakama inatoka na wapi inapotaka kuelekea hususan   katika suala zima la maboresho ya huduma ya utoaji haki nchini. Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania (2015/2016-2019/2010) umegawanyika katika nguzo kuu tatu ambazo ni utawala bora, uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali. Nyingine ni upatikanaji na utoaji haki kwa wakati na kurejesha imani ya jamii na ushirikishwaji wa wadau na umejikita katika kuboresha huduma za utoaji haki kwa ujumla. Naye Rais wa TLS, Tundu Lissu pamoja na mambo mengine   alieleza baadhi ya changamoto zinazowakabil...

Dr Slaa Ajitathimni Kurud Nchini.......Adai Upinzani Usipojipanga Unaweza Kufutika 2020

Image
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye kwa sasa anaishi nje ya nchi, Willbrod Slaa amesema anajitathmini kwa kile kilichomfanya aondoke hapa nchini na familia yake kama hakipo aweze kurejea nyumbani. Dkt. Slaa aliamua kuweka pembeni masuala ya siasa baada ya kutofautiana na chama chake juu ya masharti ya kumpokea aliyekuwa mgombea wa Urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa. Amesema kuwa kwa sasa amemaliza masomo yake na baada ya kutafakari na kujitathmini atarejea nyumbani muda wowote. “Ni kweli nimemaliza masomo yangu, bado napima mazingira yaliyonifanya niondoke na familia yangu, baada ya hapo nitaangalia uwezekano wa kurejea nyumbani,”amesema Dkt. Slaa. Aidha, kuhusu mwenendo mzima wa Serikali ya awamu ya Tano, amesema kuwa hakuna nchi hata moja ulimwenguni ambayo Rais wake atakubarika kwa asilimia mia moja, hivyo Rais Magufuli ameonyesha msimamo wa kusimamia kile anachokiamini Hata hivyo, ameongeza kuwa kama wapinzani hawat...

Mwanamitindo anayeugua 'ugonjwa wa paka'

Image
Mwanamitindo Caitin Stickels ana tatizo nadra sana la kiafya ambalo hufahamika kama 'Ugonjwa wa macho ya paka' ambalo humsababishia maumivu makali sana. Lakini bado hajakata tamaa. Tatizo hilo la kiafya humfanya aonekane kama paka. Hali yake ilimvutia mpiga picha za mitindo kutoka Uingereza Nick Knight. Alimtazama mwanamitindo huyo wa miaka 29 kutoka Seattle mara ya kwanza kwenye Instagram. Tangu wakati huo, amevuma kama mwanamitindo na hata picha zake zikachapishwa katika jarida la V Magazine. "Ni mabadiliko makubwa zaidi mema yaliyowahi kutokea katika maisha yangu," aliambia BBC. Ugonjwa huo wa macho ya paka hufahamika kitaalamu kama Schmid-Fraccaro Syndrome. Watu wenye ugonjwa huo wanaweza kuwa na matatizo katika maumbile ya masikio yao, moyo na kwenye figo. Wakati mwingine, viungo vingine mwilini huathiriwa. Sura ya Caitin si kama ya wanamitindo wengi ambao wamevuma sana. 'Urembo' wake si kama ule wengi waliozoea kuona ukiangaziwa kwenye majarida, filamu n...

Messi apigwa marufuku mechi nne kwa kumtukana mwamuzi

Image
  Nyota wa Argentina Lionel Messi amepigwa marufuku mechi nne za kimataifa kwa kumtukana mwamuzi msaidizi wakati wa mechi kati ya taifa lake na Chile siku ya Alhamisi mjini Buenos Aires . Shirikisho la soka duniani FIFA, lilitangaza uamuzi huo saa chache kabla ya Argentina kukutana na Bolivia katika mechi muhimu ya kufuzu kwa Kombe la Dunia mwaka ujao. Argentina, walionekana kumkosa sana mshambuliaji huyo wa Barcelona, na walilazwa 2-0 katika mechi hiyo iliyochezewa mji wa La Paz. Mabao ya Bolivia yalifungwa na Juan Carlos Arce na Marcelo Martins. Argentina wanakabiliwa na hatari ya kushindwa kufuzu kwa michuano hiyo itakayoandaliwa nchini Urusi. Timu nne za kwanza Amerika Kusini ndizo huhakikishiwa nafasi ya kucheza michuano hiyo. Kwa sasa, Argentina wanashikilia nafasi ya nne. Zikiwa zimesalia mechi nne za kufuzu, Colombia walipanda juu ya Argentina na Uruguay na kutua nafasi ya pili kwa kulaza Ecuador 2-0 kupitia mabao ya James Rodriguez na Juan Cuadrado. Argentina huenda wakat...

Mkenya Clifton Miheso adai kutishiwa kwa bunduki Afrika Kusini

Image
  Mchezaji wa kimataifa wa Kenya Clifton Miheso amewasilisha rasmi malalamiko katika shirikisho la soka duniani Fifa akidai kwamba alilazimishwa kwa mtutu wa bunduki kuhitimisha mkataba wake katika klabu ya Golden Arrows. Miheso anadai kisa hicho kilitokea 14 Januari katika afisi za klabu hiyo mjini Durban nchini Afrika Kusini. Mchezaji huyo wa miaka 24 anataka Golden Arrows wapigwe marufuku kununua au kuuza wachezaji au wapewe adhabu nyingine yoyote ile. Aidha, anataka alipwe jumla ya $22,000 ambazo anasema anaidai klabu hiyo kama ujira wake. Golden Arrows wamekanusha tuhuma za mchezaji huyo lakini wakakataa kuzungumzia zaidi kisa hicho. Mwakilishi wa winga huyo anasema kalbu hiyo haikutoa maelezo yoyote ya kuridhisha kuhusu kisa hicho. Miheso ameichezea timu ya taifa ya Kenya mechi 14 na kufunga magoli matano.

Sanamu ya kushangaza ya Cristiano Ronaldo yazinduliwa Ureno

Image
Mashabiki wengi wa mchezo wa kandanda dniani wameshangazwa na sanamu ya mchezaji nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo ambayo ilizinduliwa katika kisiwa cha Madeira nchini Ureno. Sanamu hiyo ilizinduliwa wakati wa sherehe ya kuupa jina uwanja wa Madeira ambao sasa umekuwa Uwanja wa Cristiano Ronaldo. Wengi katika mitandao ya kijamii wanasema sanamu hiyo inafanana sana na nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Jamhuri ya Ireland Niall Quinn badala Ronaldo. Waziri mkuu wa Ureno alihudhuria sherehe hiyo ya kuupa jina uwanja huo wa Madeira na ndiye aliyezindua sanamu hiyo.     Rais wa Ureno Rebelo de Sousa alisema Ronaldo "amekuwa akitangaza Madeira na Ureno maeneo ya mbali zaidi duniani kuliko mtu mwingine yeyote." Ronaldo, 32, huchukuliwa kama shujaa Madeira, ambapo anatazamwa kama mfano mwema kwa mtu aliyeanzia maisha katika ufukara hadi akawa tajiri. Tayari ana makumbusho yaliyopewa jina lake katika mji wake wa kuzaliwa wa Funchal. Mchezaji huyo baadaye aliandika kwenye Twi...