Mwanamitindo anayeugua 'ugonjwa wa paka'

Caitin Stickels
Mwanamitindo Caitin Stickels ana tatizo nadra sana la kiafya ambalo hufahamika kama 'Ugonjwa wa macho ya paka' ambalo humsababishia maumivu makali sana.

Lakini bado hajakata tamaa.

Tatizo hilo la kiafya humfanya aonekane kama paka.

Hali yake ilimvutia mpiga picha za mitindo kutoka Uingereza Nick Knight.

Alimtazama mwanamitindo huyo wa miaka 29 kutoka Seattle mara ya kwanza kwenye Instagram.

Tangu wakati huo, amevuma kama mwanamitindo na hata picha zake zikachapishwa katika jarida la V Magazine.

"Ni mabadiliko makubwa zaidi mema yaliyowahi kutokea katika maisha yangu," aliambia BBC.

Ugonjwa huo wa macho ya paka hufahamika kitaalamu kama Schmid-Fraccaro Syndrome.

Watu wenye ugonjwa huo wanaweza kuwa na matatizo katika maumbile ya masikio yao, moyo na kwenye figo.

Wakati mwingine, viungo vingine mwilini huathiriwa.

Sura ya Caitin si kama ya wanamitindo wengi ambao wamevuma sana.

'Urembo' wake si kama ule wengi waliozoea kuona ukiangaziwa kwenye majarida, filamu na runinga.

"Sikuwahi kuwa na ndoto ya kuwa mwanamitindo au kufikiria ningeshiriki katika tasnia ya mitindo na mavazi,"
Caitin Stickels

Comments

Popular posts from this blog

MREMBO GIGY MONEY AFANYA KUFURU NYINGINE

Hamorapa kuhusu Ishu ya kumpigia Alikiba Magoti .