Posts

Showing posts from October, 2016

Vyakula Vinavyoongeza Hamu na Nguvu ya Kufanya Tendo la Ndoa

Image
Tatizo la uwezo wa kufanya tendo la ndoa linazidi kukua miongoni wa wanandoa na wapenzi wengi. Takwimu za kitafiti zinaonyesha kuwa karibu ndoa 4 kati ya 10 zenye umri wa miaka 3 na kuendelea zinakabiliana na tatizo hili. Aidha wanaume 6 kati ya 10 wanatajwa kulalamikia upungufu wa nguvu za kiume. Pamoja na matatizo mengine kutajwa kuchangia upungufu wa nguvu za kiume na kushuka kwa msisimko wa tendo miongoni mwa wanandoa, uchunguzi umeonesha kuwa utumiaji holela wa vyakula hasa vyenye mafuta ni moja kati ya sababu zinazochangia kwa kasi tatizo hili. Kwa kuzingatia hilo, watafiti wa masuala ya uhusiano wa kimapenzi wamebaini aina mbalimbali ya vyakula ambavyo vina uwezo wa kumuongezea mtu nguvu ya kufanya tendo la ndoa.  Vyakula hivyo ni hivi vifuatavyo: 1. PILIPILI Kama tunavyojua wote mara nyingi chakula ambacho kimeungwa pilipili hufanya hata mapigo ya moyo kuwa tofauti na wakati mwingine hata jasho au kamasi hutoka. Ndani ya pilipili kuna kitu kinaitwa capsaicin ambacho hufanya...

Audio: Baba Mzazi, Francis Miyeyusho Wasimulia Kifo cha Bondia Thomas Mashali Kilivyotokea

Image
Bondia Thomas Mashali, ameuawa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira usiku wa kuamkia leo, baada ya kupigiwa kelele za mwizi kufuatia ugomvi uliozuka maeneo ya Kimara, jijini Dar es Salaam. Bondia, Francis Miyeyusho aliyekuwa mwanafunzi wake, ameiambia East Africa Radio kuwa Mashali aliumizwa vibaya kichwani. Amesema Jumapili hadi saa tisa alasiri walikuwa pamoja kwenye kikao cha masuala ya masumbwi na alimuaga kuwa anaenda Kimara. “Baadaye nikaja kusikia story kwamba kuna mtu kagombana naye pale wamemchenjia wameanza kumuitia kelele za mwizi mitaa ya Kimara huko kwahiyo wamemchangia raia, wamempiga,” amesimulia Miyeyusho. Bondia huyo amesema kuwa Mashali alikuwa amenyoa rasta zake na kwamba huenda hiyo ni sababu wananchi wengi walishindwa kumtambua. Kwa upande wa baba yake mzazi, Mzee Christopher Mashali, amesema alipata taarifa hizo usiku akiwa amelala kutoka kwa vijana wanaomfahamu. Vijana hao walimweleza kuwa mtoto wake amepigwa vibaya kiasi cha kupasuliwa kichwa na usiku huo kuwapi...

Faraja Kotta Azungumza Hili Baada ya Miss Tanzania 2016 Diana Edward Kuandamwa Mitandaoni

Image
Aliyewahi kuwa mshindi wa Miss Tanzania kwa mwaka 2004, Faraja Kotta Nyalandu amechukizwa na yale yanayoendelea katika mitandao ya kijamii juu mshindi wa taji la Miss Tanzania 2016, Diana Edward. faraja Hatua hiyo imekuja baada ya watu katika mitandao ya kijamii kuanza kumshambulia mshindi huyo juu ya umri wake. Hata hivyo kamati ya Miss Tanzania ilitolea ufafanuzi juu ya suala hilo. Miss Faraja Kotta ambaye na yeye pia alipitia kipindi kigumu pindi alipotangazwa mshindi, ameandika ujumbe huu: "Niliposhinda Miss Tanzania, kuna mtangazaji fulani (tena wa kiume) wa kipindi cha redio cha asubuhi alitumia kama saa nzima hewani kusema ambavyo sikustahili kushinda. Asubuhi ya Jumatatu kama leo baada ya weekend ya shindano. Nilipigiwa simu kuamshwa. Nakumbuka niliamka nikawasha redio na nikasikiliza kipindi chote, peke yangu, chumbani. Nilitetemeka, nilishindwa kuoga, kula, nilijifungia ndani siku nzima nikilia. Niliwaza sana ambavyo pengine ni kweli sikustahili. Nilijuta kushiriki Miss ...

HESLB Yafafanua vigezo Utoaji mikopo, Waliokosa sababu zatajwa, wapewa nafasi ya kukata rufaa

Image
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa ufafanuzi kuhusu vigezo inavyotumia katika kuchambua, kupanga na kutoa mikopo kwa wanafunzi 20,183 (asilimia 74) wa mwaka wa kwanza hadi sasa kati ya 25,717 iliyopanga kuwapa mikopo katika mwaka huu wa masomo, 2016/2017. Idadi iliyobaki (asilimia 26) ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza itajazwa na waombaji ambao baadhi ya nyaraka walizowasilisha zinaendelea kuchambuliwa ili kuthibitisha uhalisi wake na baadhi zitajazwa na waombaji ambao wanakata rufaa na kuwasilisha nyaraka zinazothibitisha uhitaji wao kwa mujibu wa vigezo vya mwaka huu. Aidha, katika mwaka huu wa masomo, Serikali imepanga kutumia jumla ya Tshs 483 kutoa mikopo kwa wanafunzi 93,295 wanaoendelea na 25,717 wa mwaka wa kwanza. Katika mkutano na waandishi wa habari jana (Jumapili, Oktoba 30, 2016), Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru alisema vigezo vikuu vinavyotumika mwongozo uliotangazwa na Bodi hiyo wakati ilipotangaza kuanza kupokea maombi mwezi Juni...

Bondia Mtanzania Dulla Mbabe ampiga mchina kwa Knockout

Image
Bondia kutoka Tanzania Abdallah Pazi Dulla Mbabe alimrambisha sakafu mwenzake kutoka China Zheng Chengbo katika pigano kali lililofanyika usiku wa Ijumaa katika ukumbi wa Diamond Jubilee mjini Dar es Salaam. Dulla iliorushwa ngumi nzito na kumwangusha mpinzani wake na kumfanya kushindwa kuendelea na pigano hilo la uzani wa Light Heavy. Dulla ambaye alianza pigano hilo kwa kasi na kufanikiwa kumwangusha bondia huyo wa China kwa sekunde kadhaa. Hatahivyo Chengbo aliamka na kuendelea na pigano. Bondia wa Tanzania alifanikiwa kumweka Chengbo katika kona na kumrushia makonde makali akimwacha akitokwa na damu chungu nzima katika pua. Ni wakati huohuo ambapo bondia huyo alishindwa kunyanyuka kutoka sakafuni ndipo refa akamaliza pigano hilo na kumpatia ushindi wa Knock-out Dulla. Bondia huyo sasa ameshinda mapigano 14 ,13 yakiwa katika njia ya Knockout na kushindwa mara tatu. Picha: Na Michuzi Blog

Show ya Diamond Malawi Yafana Licha ya Mvua Kubwa Kunyesha

Image
Licha ya mvua kubwa kunyesha, Diamond amefanikiwa kupiga show iliyofana kwenye Sand Music Festival iliyofanyika kwenye fukwe za Living stone Jumamosi hii. Mpiga picha wake, Kifesi amedai kuwa mvua kubwa ilinyesha na kulazimu show yake kusimama kwa muda. Hata hivyo mashabiki waliokuwa na hamu kumuona akitumbuiza, walisubiri hadi ilipokata. Kwenye picha hii Kifesi ameandika: Picha juu ni usiku watu wakiwa na shauku ya Diamond but mvua ikanyesha, but walingoja hadi hali ilipotulia.. Picha chini na alfajiri saa 12 hali ilipotulia na Diamond kupanda na hakuna alokua kuchoka or kuondoka Kwenye show hiyo Diamond alitumbuiza live. Hizi ni picha zaidi:

Utafiti: Kukumbatiwa na Umpendaye Wakati wa Maumivu Kuna Nguvu zaidi ya Paracetamol

Image
Kumbatio kutoka kwa mtu umpendaye, linaweza kuwa na nguvu zaidi ya Paracetamol pale unapokuwa na maumivu, kwa mujibu wa utafiti. Wanasayansi wamebaini kuwa hisia za ukaribu tunazozipata kupitia mtu anayetushika, kunaweza kusaidia kupunguza maumivu. Lakini kushikwa na mtu usiyemjua, kunaweza kusiwe na matokeo yale yake, kwasababu hatuna hisia nao. Utafiti huo unaonesha nguvu ya ubongo kuzuia hisia za maumivu. Utafiti huo ulifanywa na wataalam katika chuo kikuu cha Haifa, Israel na ulihusisha wanawake kadhaa ambao waliwatengenezea maumivu kwa kuwaunguza na chuma chenye moto kiasi. Katika jaribio la kwanza, mtu wasiyemjua aliwashika mkono akijaribu kuwaliwaza kwa maumivu hayo. Kwenye la pili waliwaita waume na wapenzi wao kukaa karibu nao na kugusanisha ngozi. Katika jaribio la mwisho, wapenzi wao waliruhusiwa kuwashika mkono wakati chuma hicho cha moto kikigusishwa kwenye ngozi zao. Wanasayansi walibaini kuwa mguso wa mtu wasiyemjua pamoja na kuwa na mpendwa wao karibu hakukuwa na tofaut...

Bibi Aliyejichongea Jeneza Afariki Dunia

Image
Mkazi wa Kijiji cha Lindusi Peramiho mkoani Ruvuma aliyejichongea jeneza, Scholastica Mhagama amefariki dunia  kwa ugonjwa wa pumu. Mapema mwaka huu wakati alipohojiwa na gazeti hili, bibi huyo alitaja sababu za kujichongea jeneza kabla ya kifo kuwa, ni kuhofia kuzikwa kama mnyama baada ya kuwa na ugomvi wa mara kwa mara na kaka zake. Kaka yake mkubwa aliyekuwa akimhudumia kabla ya kufariki dunia, Felix Mhagama (82) alisema dada yake alikufa Jumanne ya wiki iliyopita kwa ugonjwa huo. Mhagama alisema licha ya kipindi cha uhai wa dada yao, kugombana mara kwa mara walikuwa wakipatana na kumaliza tofauti zao. “Ingawa mdogo wangu alikuwa na upungufu niliendelea kuzungumza naye na kumhudumia, kwani hakuwa na uwezo wa fedha na alinitegemea kwa kila kitu,” alisema. Alisema alikuwa akiumia kuona dada yake akiishi na jeneza hilo na kwamba, kuna wakati alimuuliza sababu za kufanya hivyo, alimjibu kuwa ni kutokana na kutokuelewana kwao. Alibainisha kuwa kabla ya kifo chake, kuna watu walikwend...

WEMA Sepetu Achoshwa na Timu Wema Aanza Kuwa Block Vinara wa Timu hiyo Instagram..Aanza na Huyu

Image
Wema Aanza kuwapa Block Vinara wa Team Wema....Msikie huyu...... #Regrann from #myboowemasepetu - Msema ukweli kipenzi cha mungu. Msione najichekesha chekesha mkazani nimefurahi. Ukweli ni kwamba nimeumia sana adi chozi limenidondoka 😢 inachoma kama pasi 😭😭😭😭. Wema ulianza kumblock legend wetu katika team anaitwa @kimbwi222 iliniuma sana, leo mimi @myboowemasepetu kesho sijui nani. To be honest naumia 😢😭😭😭 un follow ilikuwa haitoshi madam ukaona unipe sollex. Umesahau mazuri yote umekumbuka baya moja tu la jana kisa kumponda aunt. Na sijamponda nimeongea ukweli sasa unataka tufagilie adi ujinga unaofanya. Wema your loosing amka kwenye huo usingizi mzito ulionao. Wanajua hakuna team inanguvu insta kama teamwema, wanakupoteza ukose mtetezi daaaaah nashindwa ata cha kuandika. Mungu mwenyewe ndo anajua kuwa ninamapenzi ya kweli kwako. Watakaonicheka na wanicheke nimeongea ukweli kutoka moyoni. Na asante sana kwa block 🙏🙏🙏🙏. Life goes on .... " MPE ushauri....

Mr Blue ataja jina analotumia baada ya ‘Simba’ kupokonywa

Image
Mr Blue amelitaja jina lake jipya analolitumia baada ya lile la ‘Simba’ kuchukuliwa na Diamond Platnumz. Rapper huyo amesema kuwa kwa sasa anatumia jina la ‘Nyani Mzee’ kama jina lake jingine la utani. “Actually kwa sasa jina la Simba nimeliacha ila kwa sasa natumia jina la ‘Nyani Mzee’ nikimaanisha nimekwepa mshale mingi. Nasubiri na hilo wachukuwe nitafute jina jingine,” amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio. Mwezi Disemba mwaka jana Mr Blue na Diamond waliingia kwenye mzozo kuhusiana na jina la ‘Simba’ huku kila mmoja akidai ni lake.

Eric Bailly atakuwa nje ya uwanja kwa miezi miwili

Image
Mchezaji wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya Ivory Coast, Eric Bailly atakuwa nje ya uwanja kwa miezi miwili baada ya kuumia goti. Hili ni pigo kwa Jose Mourinho ambaye Bailly amekuwa ni beki tegemezi katika kikosi chake cha United.

Aunty Lulu Awachana Mr Bond na Wastara...Adai Alimuokota Mr Bond Jalalani na Kumlea

Image
Bifu Jipya mjini.....Aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Mr Bond Aunty Lulu ameibuka pasipo julikana na kuanza kuwashambulia kwa maneno Mr Bond na Mpenzi wake Wastara... Ameandika haya kwenye ukurasa wake wa Instagram: Auntylulukimwana   "Nilikuokota jalalani mbwa wewe hujui hata kuvaa..ulikuja kwangu umevaa suruali kama alusi mabele au kanda bongoman wa zamani..ukaishi kwangu hata kazi huna mbwa wewe nikakutafutia mwenyewe channel 10..tena nikakuasa usije kuniacha..maana wakikuona watakutaka ukasema hatuwez kuachana...umepata kazi kwa mgongo wangu mwenzangu ukadindisha na kuwapa mti baadhi ya mastar(siwataji japo nawajua)na huyo ngedere wako kwa ujane akaamua kuwa wako..kumbuka mm ndo nilikupa taarifa ya kifo cha mumewe,,,alfajiri tumepata taarifa tulikuwa tumelala..we si ndo uliniomba turudiane ulivyoachwa akaenda kwa mbunge?nilikataa kwa kuwa nna mtu tayari!!leo hii kakurudia..utaishia hvyohvyo kukimbiwa ngoja atokee mkubwa zaidi ya mbunge yakukute..na usirudi hapa"   Amendika A...

Mahakama Yamfutia Shtaka la Unyang’anyi wa Kutumia Silaha Scorpion

Image
Mahakama ya Wilaya Ilala jijini Dar es Salaam leo imemfutia shtaka la   unyang’anyi wa kutumia silaha, Salum Njwete maarufu kwa jina la Scorpion baada ya upande wa mashtaka kuomba shtaka hilo liondolewe mahakamani hapo kwa sababu hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo. Mtuhumiwa huyo ambaye ni mkazi wa Buguruni kwa Mnyamani anatuhumiwa kumchoma visu na kisha kumtoboa macho, Said Ally mkazi wa Mabibo Hostel hivi karibuni. CHANZO: UDAKU SPECIALLY

Watu 13 Kizimbani Kwa Mauaji ya Watafiti Dodoma:

Image
Wanawake wanne na wanaume tisa wamefikishwa mahakamani mjini Dodoma na kusomewa mashtaka ya mauaji ya watafiti wa Chuo cha Utafiti wa Udongo na Maendeleo ya Ardhi kilichopo Selian mkoani Arusha. Mbele ya Hakimu Mkazi, Joseph Fovo washtakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma haina mamlaka kisheria kusikiliza kesi hiyo isipokuwa Mahakama Kuu. Wanadaiwa kuwaua Nicas Mag- azine, Theresia Nguma na Faraji Mafuru, Oktoba Mosi kwenye Kijiji cha Iringa Mvumi wilayani Chamwino. Wakili wa Serikali, Beatrice Nsana aliwasomea mashtaka hayo jana akidai walitenda kosa hilo la jinai kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu na marekebisho yake ya mwaka 2002. Washtakiwa hao ni Cecilia Mwalu, Dorca Mbehu, Edna Nuno, Grace Masaulwa, Juma Madeha, Albert Chimanga, Sosteness Mseche, Julius Chimanga, David Chimanga, Lazaro Kwanga, Yoramu Samamba, Edward Lungwa na Simon Samamba, wote wakazi wa Kijiji cha Iringa Mvumi. Kesi hiyo namba 36/2016 iliahiris...

Walimu Waipa Serikali Siku 15 Ilipe Madeni Yao

Image
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kimetoa siku 15 kwa Serikali kumaliza madai yao ya muda mrefu vinginevyo watachukua maamuzi magumu. Rais wa CWT, Gratian Mukoba amesema kuwa uvumilivu wao umeelekea kufikia ukingoni kwani wamekuwa wakikaa mezani na Serikali mara kwa mara na kupewa ahadi za kutatua matatizo yao lakini hadi sasa hazijatekelezwa. Alisema kuwa Agosti  22 na 23 mwaka huu, Baraza la chama hicho cha walimu lilipitisha maazimio kupitia kikao chake, maazimio ambayo yalisainiwa pia na upande wa Serikali kwa ahadi kuwa wangeyafanyia kazi lakini imeendelea kuwa kimya. “Siku chache baadae tuliambiwa tusubiri mchakato wa kuhakiki watumishi ukamilike. Lakini licha ya mchakato huo kukamilika Serikali imeendelea kukaa Kimya,” Mukoba anakaririwa na Tanzania Daima. Aliyataja madai hayo kuwa ni pamoja na posho ya madaraka kwa wakuu wa shule, muundo wa madaraka, walimu kutopandishwa madaraja na kulipa madeni ya walimu. “Ninachoweza kukwambia ni kwamba mwishoni mwa Oktoba ambao ...

SITTA AREJEA NCHINI KUTOKA UJERUMANI ALIKOENDA KUTIBIWA MIGUU

Image
Spika wa Bunge mstaafu, Samuel Sitta amerejea nchini kutoka Ujerumani alikokwenda kwa ajili ya matibabu ya miguu. Septemba mwaka huu, Sitta alikwenda nchini humo baada ya kusumbuliwa na tatizo hilo. Mmoja wa wanafamilia wa mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa waziri wa wizara mbalimbali serikalini, alimwambia mwandishi wa habari hizi kuwa hali yake inaendelea vizuri.  Hata hivyo mimi siyo msemaji wa familia,” alisema mtoa habari huyo. Alipotafutwa mke wa Sitta, Margaret ambaye alirithi ubunge wa Urambo kutoka kwa mumewe, alisema alikuwa benki na asingeweza kuzungumza  na simu.  

DUNIA INA MAMBO MAZITO BI HARUSI AMPA SUMU MUMEWE

Image
Msichana mdogo alieolewaBi harusi wa miaka 14 nchini Nigeria ameshtakiwa kwa kuwaua watu wanne akiwemo mumewe wa miaka 35 baada ya kuweka sumu ya panya katika chakula alichoandaa kwa sherehe za haruysi yake. Kesi hiyo imewashangaza wahaharakati wa haki za kibinaadamu ambao wamesema kuwa msichana aliyeozwa kwa mume aliye mara mbili umri wake anafaa kuchukuliwa kama mwathiriwa na wala sio muhalifu. Wasila tasiu kutoka familia masikini katika eneo la waislamu la kazkazini huenda akakabiliwa na kifo iwapo atahukumiwa. Shahidi wa kwanza wa kiongozi wa mashtaka Lamido Abba Sorron-Dinka alikuwa msichana wa miaka 7 anayejulikana kama hamziyya,ambaye alikuwa akiishi katika nyumba moja na Tasi'u pamoja na mumewe Umar sani,wakati bi haru huyo alipoweka sumu ya panya katika chakula hicho. Hamziyya alijulikana tu kama dadaake mke wa kwanza wa bwana Sani,mwanamke aliyeolewa na marehemu awali katika eneo ambapo ndoa za wake wengi zimekithiri. Msichana huyo wa miaka 7 alisema kwamba Tasi'u ali...

KAFULILA ASHINDWA KESI YA UBUNGE KIGOMA KUSINI

Image
KWA mara nyingine tena Mahakama imetupa maombi ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyofunguliwa na David Kafulila akipinga ushindi wa Husna Mwilima wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kigoma Kusini, safari hii uamuzi ukitolewa na Mahakama ya Rufaa. Katika uamuzi uliotolewa jana na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa chini ya uenyekiti wa Jaji Mbarouk Salim akisaidiwa na Jaji Bernard Luanda na Jaji Richard Mziray, mahakama hiyo imetupilia mbali rufaa hiyo ya Kafulila kwa kile ilichodai imekosa miguu ya kusimama. Mbali ya uamuzi huo, jopo hilo la majaji wa Mahakama ya Rufaa pia limemtaka mlalamikaji ambaye hawakuwepo mahakamani kulipa gharama za shauri hilo la madai namba 212/2016. Majaji hao walisema wanakubaliana na maombi ya Wakili wa Serikali Gabriel Mallata aliyepinga shauri hilo kusikilizwa kutokana na kile alichodai kwamba halikukidhi matakwa ya sheria. Hii ni mara ya pili kwa Kafulila kuangushwa kisheria katika shauri alilofungua kupinga ushindi wa mgombea wa CCM Mwilima a...

Wanawake wanaotumia kope bandia wanahofiwa kuwa na hali ya hatari ya kupata upofu wa macho

Image
Wanawake wanaotumia kope bandia wanahofiwa kuwa na hali ya hatari ya kupata upofu wa macho kutokana na gundi wanazotumiwa kutumia kope hizo kuripotiwa kuripotiwa kuwa na athari kwenye macho yao. Tahadhari hiyo imetolewa na mratibu wa huduma ya macho ya mkoa wa Iringa, Dk George Kabona,alipokuwa akitoa tathmini ya huduma ya macho ikiwa ni sehemu ya kuelekea maadhimisho ya siku ya afya ya macho duniani. “Ningependelea wasipende kuzivaa kama fasheni ya kawaida,kwasababu zina madhara sana. Kwasababu hizo kope unabandika kwa kile kitu ambacho ile chemical ya kubandikia ndio huwa inaogopwa zaidi kuliko hata kope zenyewe. Ingekuwa labda unazibana na stapler hivi labda lakini kuna kitu unabandikia ile kitu ndio jicho halikitaki kama kinaendelea kukaa pale muda mrefu,”alisema Kabona. “Pia hupelekea uoni hafifu. Pia linaweza likawapelekea watu shida ya kuona kwasababu uoni hafifu kuna ule mkali na uoni hafifu wa nafuu. Ukiwa ule mkali utakuletea shida kwenye shughuli zako za kila s...

MASKINI: Saida Karoli Aelezea Alivyotumiwa Kuwatajirisha Watu Huku Akibaki Maskini

Image
Muimbaji nguli wa Tanzania aliyetamba na vibao kama Mapenzi Kizunguzungu, Kitobero na nyingine nyingi amesema kuwa ana hofu ya kuwa na meneja kwa sasa kutokana na yaliyomsibu miaka kadhaa nyuma. Najua, kuna mameneja wazuri katika muziki wa bongo kama meneja wa Diamond Platnumz hata wa Ali kiba. Lakini kuna baadhi ya mapromota na mameneja kwa kweli nina wahofia sana. Alisema Saida Karoli. Saida Karoli ameeeleza kuwa wakati wake alifanya vizuri sana kimuziki lakini hakuona mafanikio hayo kifedha. Hayo yote ni kutokana na uongozi wake. Amesema kuwa hata sasa akipata meneja mwingine atahakikisha anajiridhisha kwanza kama anaweza kazi ndio aingie nae mkataba. Saida Karoli amesema jina lake kwenye jukwaa ni kubwa sana kuliko mafanikio aliyonayo, na hii humfanya aamini kuwa alitumika kuwanufaisha watu wengine. Nilikuwa nikilipwa fedha kidogo sana kutokana na kazi zangu za muziki. Kama mwandishi akitembelea ninapoishi Watanzania wataweza kuelewa ni nini ninazungumzia. Muziki wa Saida Karoli ba...