Posts

Showing posts from December, 2016

MAKUBWA Yafichuka Faru John

Image
 Maofi sa wa Wizara ya Maliasili na Utalii, wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), wafanyakazi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na maofi sa Taasisi ya Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) wakiwamo madaktari, wakifanya uchunguzi wa Faru John baada ya kufa katika eneo la Sasakwa Grumeti. SAKATA la kutoweka kwa faru John lililoibuliwa wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika mikoa ya Arusha na Manyara linazidi kuchukua sura mpya kila kukicha. Taarifa zilizolifikia MTANZANIA baada ya kufanya uchunguzi wa sakata hilo kwa wiki kadhaa sasa, zinaonyesha kwamba uamuzi wa kumhamisha faru huyo kutoka Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro ulihusisha mamlaka za kitaifa za Serikali. Habari kutoka vyanzo vya kuaminika zinaeleza kwamba mchakato wa kuhamishwa kwa faru John kutoka Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro kwenda Grumeti, ulianza katika eneo la Nyasirori ndani ya Hifadhi ya Serengeti Aprili 17, 2015. Uamuzi huo kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika serikalini, ulianza siku hiyo...

HIZI Ndio Sehemu 10 zenye Msisimko Mkali zaidi Kwenye Mwili wa Mwanamke

Image
  Kila mwanaume anapenda kua fundi wa tendo la ndoa akiwa faragha na mke au mchumba wake lakini bahati mbaya sana hakuna kanuni maalumu ya kumsisimua mwanamke kwani kila mwanamke ana eneo lake ambalo likiguswa anakua taabani hivyo ni wajibu wa mwanaume kulitafuta na kuligundua eneo hilo. Mazoea ya kufanya mambo yaleyale kila siku kwa muda mrefu hufanya tendo hilo la ndoa lianze kua baya na huenda ikawa chanzo  cha mtu kuchepuka kutafuta ladha zingine. Kitaalamu katika sayansi ya binadamu kuna maeneo kadhaa ambayo wanawake wote wakiguswa hupata msisimko mkali lakini msisimko hutafautiana kutokana na mwanamke husika kama ifuatavyo. 1. Kichwani; juu ya kichwa cha binadamu kuna mishipa mingi ya damu na ile ya fahamu hivyo maeneo haya yakishikwa homoni kama oxytocin na serotoinin huachiwa mwilini na kuleta msisimko mkubwa. Jinsi ya kufanya; mshike kwanzia nyuma ya sikio kisha ingiza vidole katikati ya nywele kama unamkuna kichwa bila kutumia nguvu. 2. Sikio; sikio ni sehemu yenye m...

CHID Benzi Aonekana Live Akibwia Unga..Mwenyewe Adai Uvimbe Alionao ndio Sababu

Image
  Mtandao wa Global umeripoti habari waliyoifanyia uchunguzi na hadi kufanikiwa kumnasa Chid Benz Kwenye Chumba cha Hotel anayoishi... . Mtandao huo umeripoti hivi: DAH, KUMBE CHID ANAUMWA HERNIA Aliposogea, OFM lilimlaki kwa shangwe na kumchangamkia kiasi kilichomfanya atulie, akae chini na kuanza kupiga stori kwa zaidi ya saa moja, huku mara kwa mara akilalamika kuwa anaumwa sana ugonjwa wa Hernia na pia uvimbe chini ya kitovu ambao unamsababishia maumivu makali.  Chid alikuwa ameshika karatasi mkononi iliyoandikwa namba za simu za prodyuza Lamar ikadondoka chini, katika hali ya kushangaza alishindwa kuiokota maana kila alipoinama alihisi maumivu makali. OFM wakamsaidi a kuokota karatasi hiyo. . Chid: Washikaji msione nipo hivi lakini kiukweli ninaumwa sana, ninaweza kufa muda wowote, huu uvimbe chini ya kitovu unaniuma sana (akatoa wembe na kutaka kuuchana huo uvimbe, OFM mmoja alimdaka na kumsihi asifanye hivyo, akakubali baada ya kubembelezwa kwa muda). . ...

DHAMANI ya Mbunge Godbless Lema Yakwaa Kisiki Tena..Arudishwa Rumande

Image
  Mbunge Godbless Lema amerejeshwa tena rumande leo baada ya rufaa yake ya kupinga kunyimwa dhamana kushindikana kusikilizwa kama ilivyokuwa imepangwa katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha leo. Rufaa hiyo ya Lema iliyokuwa umepangwa kusikilizwa leo imeshindikana baada ya upande wa Jamhuri kukata rufaa kupinga kuongezwa muda wa kuwasilisha notisi ya rufaa. Upande wa mtuhumiwa uliongezea muda wa kuwasilisha notisi ya kukata rufaa kupinga kunyimwa dhamana baada ya kushindwa kufanya hivyo katika muda uliokuwa umepangwa awali. Mbunge Godbless Lema ambaye alikamatwa Novemba 2 mwaka huu mjini Dodoma amerejeshwa rumande katika gereza la Kisongo jijini Arusha.

MAAJABU: Nyoka Afa na Mmiliki wake Songea

Image
              Mkazi wa Mtaa wa Mateka, Manispaa ya Songea, Denis Komba (26) kufa baada ya nyoka wake aliyekuwa amembeba kwenye mfuko wa jaketi kuuawa na wananchi. Komba alifariki dunia katika hospitali ya Rufaa Songea mkoa wa Ruvuma (Homso) ambako alilazwa baada ya watu wenye hasira kumuua kwa mawe na fimbo nyoka wake huyo. Mashuhuda wanaeleza kuwa kabla ya wananchi kumuua nyoka huyo, Komba aliwasihi wasifanye hivyo kwa kuwa wakimuua na yeye angekufa, lakini ombi lake hilo halikusikilizwa. Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, siku ya tukio Komba alikodi pikipiki ya Kassian Haule (24) ambaye ni mkazi wa Mpitimbi, yenye namba za usajili MC 724 AKB ili apelekwe nyumbani kwake mtaa wa Mateka. Akisimulia tukio hilo, alisema alipofika katika eneo la Benki ya Posta ya zamani barabara kuu ya Sokoine, dereva wa pikipiki alihisi kuna kitu kinamtekenya na kumgonga gonga kwa nyuma, ndipo alipogeuka nyuma na kumwona abiria wake amebeba nyoka mkubwa huku amesimami...

MAPYA Yaibuka Mtoto Aliyefia Bwawani Hotelini

Image
  SAKATA la mtoto wa miaka 12 aliyekufa wakati akiogelea katika bwawa la hoteli ya kitalii ya Mount Meru mjini hapa, limechukua sura mpya baada ya kugundulika kuwa bwawa hilo lilijaa damu baada ya kifo chake. Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Charles Mkumbo amethibitisha madai ya mashahidi waliokuwa eneo la tukio, waliodai kuwa bwawa la kuogelea la hoteli hiyo liligeuka kuwa dimbi la damu wakati mwili wa mtoto huyo ukiopolewa kutoka bwawa hilo, siku ya Krismasi. “Inaaminika kuwa kichwa cha Clifford Alex kilipasukia ndani ya bwawa la kuogelea,” alisema, kamanda huyo wa Polisi wakati akitolea ufafanuzi kifo hicho kilichozua utata mjini hapa. Kuna madai kwamba Clifford alijirusha kwenye dimbwi ili aogelee, lakini kichwa chake kilipiga kwenye ukingo wa bwawa hilo la kuogelea na hivyo kusababisha kifo chake, ingawa baadhi ya watu wanadhani kuwa alisukumwa. Uongozi wa hoteli ya Mount Meru pia haujatoa tamko rasmi kuhusu tukio hilo na kwa nini watoto waliruhusiwa kuogelea bila ya kuwa na m...

FAHAMU Namna ya Kuishi na Mpenzi Anayependa Fedha...

Image
  HAPA tunazungumza kuhusu mapenzi kama kawaida yetu. Leo nimekuja na mada ambayo naamini itawagusa wengi. Marafiki zangu, kusaidia katika mapenzi ni jambo zuri tena lenye mantiki sana. Suala la kusaidiana si la upande mmoja. Linaweza kuwa kwa wote, kwa mwanaume au mwanamke. Ni kati ya nguzo muhimu katika mapenzi, lakini kwa bahati mbaya kuna wale ambao wamekuwa na tabia ya kupenda sana fedha! Unajua wenzi wanajuana kulingana na wanavyoishi, hivyo ni rahisi sana kumgundua mwenzako kama anapenda sana fedha au ni kweli ana tatizo linalohitaji msaada wako. Hii ni kasoro, lakini haimaanishi kwamba ndiyo sababu ya kuachana. Katika mada hii ipo dawa ya namna ya kudumu katika mapenzi motomoto na mwenzi wa aina hii. Imekuwa ni kawaida kumsikia msichana akitamba mbele ya wasichana wenzake kwa kusema: “Mimi nina kibuzi changu bwana kila ninachotaka kinanipa, kinajua kisiponipa nakitosa tu, yaani nakichuna kama sina akili nzuri.” Umewahi kukutana na maneno ya aina hii? Bila shaka jibu ni ndiy...

MKULIMA Aliyechomwa Mkuki na Wafugaji Apata Nafuu Baada ya Mkuki Kutolewa

Image
  Maendeleo Ya Ndugu AUGUSTINO MTITU aliyejeruhiwa kwa kuchomwa na mkuki jana tarehe 25/12/2016 Kijiji cha Dodoma Isanga Kata Ya Masanze Jimbo La Mikumi na jamii ya wafugaji, hivi sasa anaendelea vizuri na matibabu baada ya kutolewa mkuki mdomoni salama salimini kwenye HOSPITALI YA MKOA MOROGORO na amelazwa wodi namba moja hospitalini hapo. Ofisi Ya Mbunge Jimbo La Mikumi inatoa shukrani zake za dhati kwa Madaktari na wauguzi waliofanikisha zoezi hilo, Lakini pia Ofisi Ya Mbunge Mikumi itakuwa ikiwapa maendeleo ya Bwana AUGUSTINO MTITU mpaka hapo hali yake itakapokua imetengemaa. Lakini la muhimu zaidi Mh. Mbunge amefanya mawasiliano na ngazi mbalimbali zinazohusika akiwemo Waziri wa Mambo Ya ndani Mh. Mwigulu Nchemba juu ya kile kilichotokea na waziri amesikitika sana na ameahidi kulifuatilia suala hili kwa kina na kulitolea maamuzi magumu. Imetolewa na :- Robert A. Galamona Katibu Ofisi Ya Mbunge Jimbo La Mikumi

MOTO Wateketeza Nyumba 50 Wamiliki Wake Wakila Krismasi

Image
  MOTO mkubwa umezuka na kuteketeza nyumba zaidi ya 50 katika kisiwa cha Kasalazi kilichopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa mkoani Mwanza. Tukio hilo lilitokea juzi saa 3:00 usiku, linadaiwa kuwa ni la nne kutokea kisiwani humo katika miaka ya karibuni. Imeelezwa kuwa moto huo ulizuka na kuteketeza nyumba hizo huku wamiliki wake wakiwa kwenye shamra shamra za Krismasi. Nyumba zilizoteketea kwa moto ni zile zilizojengwa kwa kutumia mabanzi ya miti, mbao na kuezekwa kwa maturubai, nyasi na baadhi kwa bati.Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika. Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kasalazi, Andrew Mkama, amesema  kuwa wakati tukio hilo linatokea, wakazi wengi wa kisiwa hicho walikuwa kwenye kumbi mbalimbali za starehe kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo zaidi ya miaka 2,000 iliyopita. Mkama alisema alilazimika kupuliza filimbi kuashiria hatari na wananchi walijitokeza na kuanza jitihada za kuuzima moto huo licha ya kwamba tayari ulikuwa umeshasababisha madhara makubwa kwa kuun...

MWANAFUNZI Anusurika Kifo Baada ya Kukatwa Mapanga na Mwalimu

Image
  MWANAFUNZI Marco Limbe(14) aliyemaliza darasa la saba mwaka huu katika shule ya msingi Yitwimila iliyoko kata ya kiloleli wilaya ya Busega mkoani Simiyu amelazwa katika kituo cha afya Busega mara baada ya kuchalangwa mapanga kichwani na mdomoni na mwalimu wake. Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 11.30 jioni wakati mwanafunzi huyo alipokuwa akirejea nyumbani kwao akitokea katika malisho ya mifugo ndipo alipokaribia katika shamba la mwalimu Pendo Gabriel ndipo mwalimu huyo alimkamata kijana huyo na kuanza kumchalanga kwa panga na kupelekea kijana limbe kupoteza fahamu kwa muda wa masaa 6 mara baada ya kufikishwa katika kituo cha afya Busega. “Shuhuda wa tulio hilo aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Manoga anaeleza kuwa ilikuwa kama mchezo lakini kumbe ni kweli kwani niliona mifugo ya limbe iliyokuwa ikielekea nyumbani na huku limbe akiwa nyuma ya mifugo hiyo katika barabara ambalo liko karibu na maeneo ya shule ghafla nilimuona mwalimu pendo wakishikana na kijana huyo na nd...

CHID BENZI Anastahili Kuombewa..Siwezi Muhukumu-Solo Thang

Image
  Msanii mkongwe wa muziki wa hip hop, Solo Thang ameposti video akiwa na rapa Chidi Benz ambaye walikutana usiku na kuongea baadhi ya mambo, lakini kutokana na hali aliyokuwa nayo Chidi Benz Solo Thang alisema hawezi kumuhukumu bali anastahili kuombewa tu. Katika ujumbe ambao Solo Thang aliandika kwenye mtandao wake wa Instgram alisema hawezi kuhukumu na hata iweje bado Chidi Benz ataendelea kuwa mdogo wake, rafiki yake na mtu wake wa karibu.

RAIA 20 WAUWAWA KIKATILI MASHARIKI MWA DRC CONGO.

Image
  Takriban raia 20 wameuawa katika mauaji ya kikatili katika jimbo la Kivu ya Kaskazini nchini Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, kulinga na taarifa zilizotolewa na maafisa Jumapili. Vifo hivi ni vya hivi karibuni katika wimbi la miaka miwili la ghasia katika jimbo hilo. Mauji hayo yametokea katika mji wa Eringeti, uliopo kilomita 55 kaskazini mwa mji mkuu wa jimbo hilo wa Beni, mji ambao umekuwa ukikumbwa na misururu ya mashambulio ambayo tayari yamesababisha vifo vya raia 700, kulingana na afisa katika mkoa huo Amisi Kalonda, ambaye amewalaumu waasi kutoka Uganda kwa mashambulio ya hivi karibuni. Maafisa wa Kongo wamekuwa wakiwalaumu waasi wa ADF kwa mauaji hayo , lakini ripoti kadhaa za wataalam zimekuwa zikisema kuwa makundi mengine, yakiwemo ya wanajeshi wa serikali yalihusika katika baadhi ya mauaji. Msemaji wa jeshi la Kongo Mak Hazukay amethibitisha shambulio, akisema wanajeshi ''waliwauwa waasi wa ADF " lakini akaongeza kuwa " idadi ya raia waliokufa ni kubwa...

MPAMBANO WA WACHEZAJI

Image
  .Sio muziki hata wachezaji pia kuna mpambano wachezaji ambao kwa wanamichezo tunasema mpambano wa wasanii leo hii tunawakutanisha . SERGIO AGUERO DHIDI YA DIEGO COSTA Wote hawa wanacheza sehemu moja ya kwa maana wanacheza nafasi ya ushambuliaji kila mmoja anacheza kwa uwezo wake na umahiri mkubwa hivyo kila mmoja apewe nafasi yake na heshima yake kama mshambuliaji. DIEGO COSTA Anauwezo wa kufunga pale anapopata nafasi ya kufunga magoli yake mengi hajawahi kufunga nje ya 18 mengi akiwa ndani lakini yanaleta faida kwa timu kwa sasa ana magoli 13 na ndiye anayeongoza kwa ufungaji wa mabao pale Chelsea na EPL . Udhaifu wake nikuwa na hasira sana pindi anapokuwa na ghadhabu ila kidogo msimu huu amepunguza na ndio maana anafanya vizuri sana kikosini. Je nani unamuona mkali kati ya hao kwa kuzingatia uwezo  wake na nani unamuona anafaa ? Sina jibu sahihi wewe utaweza kuwa jaji uli useme nani zaidi.????

LUSEKELO ATIMUA WAANDISHI WA HABARI KANISANI KWAKE

Image
  MCHUNGAJI wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako, aliwagomea waandishi wa habari kusikiliza hotuba yake ya ibada na kutuma wasaidizi wake wawaondoe waandishi hao. “Samahani tunaomba muondoke kwani Mchungaji amesema hataki kumuona mwandishi hivyo tunaomba muende kwenye makanisa mengine,” alisema msaidizi huyo na kuhakikisha waandishi wote wanaondoka eneo hilo majira ya saa sita kasoro mchana. Lusekelo maarufu Mzee wa Upako hivi karibuni amekuwa akirushiana maneno na baadhi ya waandishi wa habari baada ya kuandikwa akituhumiwa kuwa mlevi na kutukana hadharani. Desemba 25 ya kila mwaka, waumini wa dini ya Kikristo nchini huungana na wenzao duniani kuadhimisha sherehe za kuzaliwa kwa Bwana wao Yesu Kristo yapata miaka 2000 iliyopita. Wakati huohuo waumini wa dini ya Kikristo nchini wametakiwa kudumisha upendo, utii na unyenyekevu ili kuadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Bwana na Mwokozi wao Yesu Kristo ikiwa ni pamoja na ...

HAJI Manara Amemmisi Jerry Muro Katika Soka...Amuombea Msamahaa TFF

Image
December 25 2016 mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Club ya Simba Haji Manara alitumia ukurasa wake wa instagram kuandika ujumbe kwa Rais wa TFF Jamal Malinzi kumuomba asamehewe afisa habari mwenzake wa Yanga Jerry Muro ambaye amefungiwa mwaka mmoja kujihusisha na soka. Kwako Rais wa TFF Kwanza nikutakie heri na baraka ktk sikukuu hii kubwa kabisa duniani kote. Nnakuandikia ujumbe huu mfupi na wa wazi kwako, nikiamini wewe ni mtu mwelewa na mwenye huruma na upendo, pia ni kiongozi mwenye maono ya dhati kwa maendeleo ya soka nchini, kwa vigezo hivyo na ukizingatia leo tupo ktk sherehe ya Noeli, utalikubali ombi langu binafsi ntakalokuomba. Nimekaa nimetafakari sana, nimeamua kumuombea msamaha mtani wangu Jerry Muro ambaye TFF mlimfungia mwaka mmoja kujihusisha na mpira wa miguu, nnafanya hivi nikijua kabisa Jerry alikosea na tayari ameshatumikia karibia nusu ya kifungo chake. Ninajua kwa kufanya hivyo atakuwa keshajifunza lugha za kutumia na pia itakuwa fundisho kwetu sis...

EDWARD Lowassa Aitaka CCM isome Alama za Nyakati

Image
  Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ameitaka CCM iache kujidanganya kuwa haiwezi kuondoka madarakani akiitaka iangalie alama za nyakati hasa mabadiliko ya uongozi yanayotokea kwingineko duniani. Hata hivyo, Lowassa ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema amesema unahitajika muungano wa dhati wa vyama na uliopangiliwa vizuri katika juhudi za kuiondoa CCM madarakani. Lowassa alisema hayo alipoombwa na mwandishi wa habari hizi kutoa tathmini ya maisha yake ya kisiasa mwaka mmoja na nusu tangu alipojiondoa CCM na kujiunga na Chadema ambako aliteuliwa kuwa mgombea urais wa chama hicho akiwakilisha muungano wa vyama vine – Chadema, CUF, NCCR - Mageuzi na NLD – Iliopewa jina la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

NDEGE Yapotea Angani na Abiria 91

Image
  Ndege ya Jeshi la Urusi, Tu-154 iliyokuwa ikielekea Syria yapotea kwenye Rada muda mfupi baada ya kupaa. Ilikuwa na abiria 91. Asilimia kubwa ya waliokuwa kwenye ndege hiyo ni Wafanyakazi wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi

Maxence Melo Afunguka "Mtandao wa Jamii Forums Haujatetereka Bado Upo Ngangari"

Image
Baada ya kuchiwa leo kwa dhamana Mwanzilishi mwenza wa JamiiForums, Maxence Melo amesema mtandao wa JamiiForums haujatetereka na bado uko ngangari na amewataka watumiaji wote wa mtandao huo waondoe hofu kwa kuwa taarifa zao za siri ziko salama. Pia amesema hana ugomvi wowote na vyombo vya dola na ana imani na mahakama za hapa nchini kuwa zitamtendea haki katika kesi yake. Amewataka wananchi wote bila kujali itikadi zao kuendelea kupigania uhuru wa kusema na kutoa maoni, pia amevishukuru vyombo vyote vya habari na wanahabari kwa kumuunga mkono kipindi chote alipokuwa mahabusu.

SERIKALI Yapiga Marufuku Shule Binafsi Kufanya Mitihani ya Kuchuja Wanafunzi

Image
  Hiyo ni baada ya kutangaza kupiga marufuku utaratibu wa kuwachuja wanafunzi wanaotakiwa kufanya mitihani ya taifa uliokuwa unaofanywa na baadhi yao kwa lengo la kuonekana shule zao zinafaulisha vizuri. Hivi karibuni, Nipashe iliripoti kuhusu hofu ya baadhi ya shule hizo; za msingi na sekondari ziko hatarini kubadilishwa matumizi kutokana na kukosa wanafunzi wa kutosha baada ya Serikali kuboresha shule zake na kutoa elimu bure, huku hali ya kiuchumi ikiwaumiza wananchi. Huku udahili kwenye shule za serikali ukiongezeka na kuonekana kuwa tishio kwa ustawi wa shule za watu na taasisi binafsi, imewabana tena wamiliki wa shule binafsi kwa kuwazuia kufanya mchujo wa wanafunzi wanaoingia kwenye madarasa au vidato vyenye mitihani ya taifa. Mmoja wa wazazi aliliambia Nipashe kuwa mwanawe anayesoma kidato cha tatu katika shule moja ya binafsi jijini Dar es Salaam, amepangiwa kuhamishiwa shule nyingine ya mmiliki huyo huyo kutokana na kufaulu kwa daraja la tatu. Kwa mujibu wa mzazi huyo, ku...

MBOWE Aeleza kwa nini Amekuwa Kimya Kupotea kwa Ben Saanane

Image
  Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema amekuwa kimya muda mrefu kuhusiana na kupotea katika mazingira ya kutatanisha, msaidizi wake Ben Saanane kwa kuwa suala hilo lipo kwenye uchunguzi. Mbowe alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Mbeya wakati wa uchaguzi wa viongozi wa chama hicho Kanda ya Nyasa inayojumuisha mikoa ya Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe na Rukwa. Alisema yeye pia ameathiriwa na tukio hilo kama ilivyo kwa wazazi wake na ndugu wengine kwa kuwa ni mtu muhimu kwake katika kutekeleza majukumu yake. “Ndugu zangu Watanzania msione nipo kimya, nimefanya hivi kutokana na kuwa suala hili lipo kwenye uchunguzi kwani tukizidisha kuongea ongea wale ambao wamemteka wanaweza kupoteza uhai wake kisa maneno,” alisema Mbowe. Alisema, “Chadema ni taasisi ambayo ina vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo vinaendelea kuchunguza tukio hili la aina yake.” Katika hatua nyingine, Mbowe aliishitumu Serikali akidai kwamba imeendelea kuwafunga wanachama wake n...

WIZARA ya Elimu yatoa ufafanuzi kuhusu ajira za Walimu

Image
  Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi imesema haihusiki na utoaji wa ajira za walimu nchini, isipokuwa inachokifanya ni uhakiki wa taarifa za walimu wenye sifa za kuajiriwa serikalini. Akizungumza nakituo cha  EATV leo, Naibu Waziri wa Elimu, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa kwa sasa wizara hiyo inapitia taarifa (CV) za walimu waliohitimu ngazi ya Stashada na Stashahada, na baada ya hapo itazituma taarifa hizo katika Wizara ya Utumishi ambao ndiyo wanaohusika na kuajiri. Akizungumzia sababu za kuwatenga wahitimu wa ngazi ya cheti, Manyanya amesema uhitaji mkubwa uliopo kwa sasa ni kwa walimu wa sekondari hususani wa masomo ya Phisics, Hisabati, Chemistry na Biolojia, hivyo inawahitaji kwa haraka zaidi walimu hao huku akisema wahitimu wengine ambao siyo wa masomo hayo na ambao siyo kwa ajili ya kufundisha sekondari, wasubiri utaratibu wa wizara inayohusika na utumishi. "Siyo kwamba hatuhitaji walimu wa shule za msingi, lakini uhitaji mkubwa tulionao ...

MAPENZI yaoneshe kwa VITENDO nasio MANENO

Image
Kama ilivyo mambo mengine kuwa na ubunifu ni swala la kujifunza, baadhi ya wanaume waliokuzwa/kulia kwenye jamii yenye mfumo Dume (Waafrika kwa ujumla) huwa hawajui kuonyesha hilo hitaji, ebu tuliite “kupenda kwa vitendo” hivyo huenda sio kwamba hataki bali hajui. Kwa maana hiyo sio mbaya ikiwa wewe mwanadada ukamfundisha nini cha kufanya, ikiwa na wewe ulikuwa hujui basi jifunzeni wote ili kuwa na uhusiano bora wenye furaha  kwa kufuata haya mambo machache ambayo wanawake wengi huwa wanapenda kufanyiwa ili wajue kweli wanapendwa kihisia na kivitendo. 1-Hakuna kitu wanawake wanazimia kama kukumbatiwa na kupigwa busu mara kwa mara. 2-Kabla hujakurupuka kitandani hakikisha umekumbatia na kubusu hata kama kalala(hakuna raha kama kuamshwa na busu au mkumbatio). 3-Mwambie jinsi gani unampenda na unavyopenda chapati/mayai/viazi alizopika au hata jinsi alivyoandaa mlo wa asubuhi. 4-Wakati unatoka ndani kumbatia chap-chap na busu kiduchu ndio utokomee kazini, hata kama mnatoka wote kwenda ...

MWAROBAINI wa EBOLA wapatikana.

Image
  Majaribio ya chanjo ya ugonjwa wa Ebola yamebainika kuwa yana uwezo na nguvu zaidi dhidi ya virusi vya ugonjwa huo hatari. Majaribio yake yamefanywa nchini Guinea, mojawapo ya mataifa ya Afrika Magharibi ambayo yalikumbwa na mlipuko wa ugonjwa huo, ambao ulimalizika mwaka huu. Matokeo ya mwisho ya majaribio hayo, yaliyochapishwa kwenye jarida la masuala ya matibabu linalochapishwa nchini Uingereza, The Lancet, yanaonyesha kuwa takriban watu elfu sita waliopata chanjo hiyo, walionekana kuwa bila ugonjwa huyo siku kumi baadaye. Miongoni mwa kundi lingine kama hilo, ambao hawakupewa chanjo, watu 23 walipatikana na virusi vya Ebola. Mkurugenzi mkuu wa taasisi moja ya matibabu nchini Uingereza- Wellcome Trust, ameelezea matokeo hayo kama ya kufana mno. Watu 11,000 walifariki wakati wa mlipuko wa hivi majuzi kwa ugonjwa wa Ebola Afrika Magharibi.

DIAMOND na Timu yake Kuchoma Gari Moto Jukwaani Kesho Wasafi Beach Party

Image
  Kama Kichwa cha habari kinavyojieleza Meneja wa Diamond Sallam Sk Mendez Akihojiwa na XXL leo Live pale mlimani City amesema wanapanga kupandisha gari Jukwaani na kulipiga kiberiti live watu wakishuhudia siku ya kesho Kwenye Party ya Wasafi ... Amedai stunt kama hizo zinasaidia kufanya mziki wetu uendelee kuwa gumzo Afrika na kukua zaidi..... CHANZO: UDAKU SPECIAL

TATU Bora Mchezaji Bora Afrika Zatoka

Image
Mshambuliaji raia wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang, mshambuliaji na winga wa Algeria Riyad Mahrez na winga wa Senegal  Sadio Mané wameingia kwenye orodha ya wachezaji wattau bora wa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika. Wachezaji hao watatu wamefika hatua hiyo baada ya kupigiwa kura na makocha na wakurugenzi wa ufundi wa vyama vya soka vilivyokuwa chini ya  CAF, kamati za vyombo vya habari, kamati za soka na ufundi na wataalamu wa habari. Mohamed Salah na Slimani hawajafanikiwa kuingia katika hatua hii. Kwa mchezaji bora wa Afrika kwa ligi za ndani, golikipa wa Uganda Dennis Onyango na Mzimbabwe Khama Billiat na mchezaji wa Zambia kiungo Rainford Kalaba wameingia. TWashindi watatangazwa kwenye tuz hizo maarufu kama Glo-CAF Awards Gala siku ya Alhamis, 5 January 2017 jijini Abuja, Nigeria. Mchezaji bora wa Afrika Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon & Borussia Dortmund) Riyad Mahrez (Algeria & Leicester City) Sadio Mané (Senegal & Liverpool) Mchezaji bora wa Afrika kwa wa...

HII ni Moja ya Zawadi Alizopewa Samatta Siku ya Birthday

Image
  Leo ni siku ambayo Mbwana Samatta anasherekea siku yake ya kuzaliwa na watu wengi wakiwemo mashabiki zake wamemuonyesha love kumtakia maisha mema na mafanikio kwenye safari yake ya soka. Kama ilivyo desturi ya watu kupewa zawadi mbalimbali siku ya birthday zao basi imekua hivyo hivyo kwa Sama Goal. Akiwa kwenye muendelezo wa safari ya kuelekea kwenye mafanikio ya soka lazima mtu kama Samatta anahitaji inspiration ya wachezaji wakubwa waliofanikiwa kwenye soka. Zawadi aliyopewa ya kitabu cha nguli Pirlo ni zawadi muhimu sana. Kitabu hicho ambacho kinaitwa “I Think Therefore I Play” kinaelezea maisha ya Pirlo aliyopitia hadi kufika alipofika leo. Maamuzi ya busara na makosa aliyofanya kwenye maisha yake ya soka yote kazungumzia humo. Kwa mchezaji kama Sama Goal ambae safari yake kwenye soka la Ulaya bado changa kitampa muongozo mzuri wa kufanya maamuzi sahihi kama Pirlo au kutofanya makosa ambayo Pirlo amefanya. Moja ya sehemu Pirlo amezungumza ni kuhusu sehemu ya maisha yake ya ki...

Miss Tanzania- ‘All along Miss Kenya was a fake friend’

Image
  Miss Tanzania, Diana Edwards recently came back with all smiles after the Miss World competitions. On a follow up, we all knew she was very social and jovial with all beauty pageants. However she was quite disappointed to find out that Miss Kenya, who she thought was a close friend, stabbed her on the back. Her documentary, ‘Maasai Dondosha Wembe’ took the position at top twenty four and she was to hold position one for Beauty With Purpose competition, but apparently Miss Kenya complained she did the same project. “I am not happy with what she did, I asked her if she knew some Kenyan designer she denied yet she has ever been designed by him. So I wore his design not knowing she has ever worn it and did a photo-shoot with it. All along she was a fake, going behind my back, saying as Africans we have to support each other yet she knew exactly what she was up-to,” said Diana.

Wabunge wa Kenya wadaiwa kuchapana makonde Bungeni

Image
   Wabunge wa upinzani nchini Kenya wametoka bungeni kwa hasira katika mji mkuu wa Nairobi, wakisema kuwa baadhi yao walinyanyaswa bungeni mapema asubuhi. Kikao hicho maalum ambacho vyombo vya habari havikuruhusiwa kuingia kilitarajiwa kupigia kura marekebisho ya sheria ya uchaguzi ambayo inaruhusu kuhesabiwa kwa kura moja baada ya nyengine katika uchaguzi wa urais mwaka ujao. Serikali inataka mfumo ambao utasaidia shughuli ya kuhesabu kura iwapo mfumo wa kielektroniki utafeli lakini upinzani unasema kuwa ni njia moja ya kuiba kura. Awali hatua ya kuupigia kura mswada huo ili ufanyiwe marekebisho ilisababisha kuzuka kwa ghasia siku ya Jumanne. Upinzani wa CORD umesema kuwa mmoja ya wabunge wake alivuja damu usoni kufuatia mgogoro na wabunge wa chama tawala mapema siku ya Jumatano. Cord imeenda mahakamani ikitaka marekabisho hayo kutopitishwa bungeni lakini chama tawala kimepitisha marekebisho hayo. Source:BBC

Dereva bodaboda akatwa sikio kwa tuhuma ya kufumaniwa na mke wa dereva teksi

Image
  Dereva bodaboda wa Mji Mdogo wa Qatesh wilayani Hanang’ Mkoa wa Manyara, amekatwa sikio kwa kisu kwa tuhuma za kufumaniwa akiwa na mke wa dereva wa teksi. Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi, Francis Massawe alisema tukio hilo lilitokea Desemba 21 saa 6:10 usiku kwenye Kitongoji cha Qendangonyi, Kata ya Ganana wilayani Hanang’. Kamanda Massawe alisema chanzo cha tukio hilo ni wivu wa mapenzi na majeruhi amepata kilema cha maisha baada ya sikio kutolewa. Alisema wanamshikilia dereva teksi kwa uchunguzi wa tukio hilo kabla ya kumfikisha mahakamani. Source: Mwananchi

MANENO ya Mourinho Kuhusu Kubakia Man United Kama Atapewa Mkataba Mpya

Image
  Kocha wa klabu ya Manchester United Jose Mourinho amefunguka kuwa anataka kubakia katika kalbu hiyo kwa muda mrefu zaidi kwa kuwa anapenda maisha yake na timu hioyo. Mourinho ambaye kwsasa ana umri wa miaka 53, alijiunga na klabu hiyo mwezi Julai, na sasa wako katika nafasi ya sita katika jedwali la ligi baada ya mechi 17. Najua kwamba ipo siku moja wataleta mkataba mpya, nitatia saini. alisema Mourinho wakati akingea na waandishi. Mourinho pia amesema kwamba hatoelekea kufanya kazi nchini China , japokuwa amekiri kwamba fedha za China zinavutia kila mtu. Nataka kusalia katika timu yenye changamoto kubwa ya kujipatia ushindi

ROBOTI Inayoweza Kushiriki Ngono Kutengezwa

Image
  Hii teknolojia sasa imekuwa too much! Kila kukicha wenzetu wazungu wamekuwa wakibuni vitu vipya tofauti kabisa na fikira za kawaida za kibinadamu na kuendelea kuushangaza ulimwengu na viumbe vyake, hatujui tunaelekea wapi na hizi teknolojia zinazobuniwa na wenzetu kila siku. Je ungependelea kushiriki ngono na roboti? Ungefunga ndoa na roboti? Je roboti anaweza kuwa na haki ya kupinga ndoa hiyo? Haya ni baadhi ya maswali machache yanayoulizwa katika mkutano wa pili wa kuwa na mpenzi wa roboti mbali na kushiriki naye ngono katika Chuo Kikuu cha Goldsmith mjini London nchini Uingereza baada ya Serikali ya Malaysia ambayo ndio iliokuwa taifa la maandalizi ya mkutano huo kuupiga marufuku. Hatua hiyo imezua utata sio tu kwa mataifa yenye maoni ya Kihafidhina na hapakuwepo na wawakilishi kutoka kwa sekta ya ngono wala roboti za ngono katika mkutano huo. Kampuni ya Real Dolls inayotengeza wanaserere wa ngono (roboti) ilidai kwamba itatengeza roboti wanaoweza kushiriki ngono na ...

MKUU wa Wilaya Mdogo Kuliko wote Tanzania na Sifa za Mwanaume Anayetamani Kuolewa naye

Image
  Zainab Abdallah, Mkuu wa wilaya ya Pangani ndiye kiongozi wa nafasi hiyo mwenye umri mdogo kuliko wote Tanzania, kwa sasa Zainab ana miaka 23 tu na bado hajaolewa lakini pia anazo sifa anazohitaji kutoka kwa mwanaume anayetamani kuolewa nae. AYO TV na millardayo.com imempata Zainab Abdallah kwenye Exclusive na ameeleza jinsi anavyokutana na maswali mengi kuhusu lini ataolewa, nani ataolewa naye na je atakuwa na sifa zipi ili waendane. “Nahisi nahitaji kuolewa na hata baadhi ya viongozi wameniambia Zainab utafika mbali sana lakini una mtihani mmoja tu unahitaji kuolewa, hilo ndio swali kubwa naulizwa. Unajua mimi ni binti mdogo lakini nimepanda sana kwenye siasa.” “Kuna wakati nafikiria kuolewa na mwanaume ambaye hayuko kabisa kwenye masuala ya siasa, kwasababu tutaweza kuiweka sawa familia wakati mimi napokuwa kwenye kazi yeye atakuwa na muda na watoto, wakati mimi niko na watoto yeye atakuwa kwenye siasa, mwanaume ambaye ni mfanyabiashara labda au meneja wa taasisi f...

POLISI Agoma Kumtaja ‘Dikteta Uchwara’ Kizimbani

Image
  ASP Kimweli, Mratibu Msaidizi wa Jeshi la Polisi ambaye ni shahidi wa pili katika kesi inayomkabili Tundu Lissu Mbunge wa Singida Mashariki, amepata kigugumizi cha kumtaja diktekta uchwara katika ushahidi wake, anaandika Faki Sosi. Tundu Lissu anatuhumiwa kufanya uchochezi akisema “Dikteta uchwara” anapaswa kupingwa na watu wote. Akitoa ushahidi wake leo, ASP Kimweli mbele ya Godfrey Mwambapa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi kisutu alieleza kuwa terehe 28 Juni mwaka huu katika viwanja vya mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu alimsikia Lissu akitoa maneno ya uchochezi. Akiongozwa na Mohammedi Salum wakili wa Serikali alidai kuwa alimshudia Lissu akitoa maneno ambayo yangeweza kuwashawishi wananchi waipinge serikali yao. Baada ya ASP Kimweli kueleza hayo ,Peter Kibatala wakili wa upande wa utetezi alimuuliza Shahidi huyo kuwa Dikitekta uchwara ni nani? Ndipo aliposema hamjui. Kibatala : Ni sahihi kuwa unayoyaongea Mahakamani, mliyajadili na wakili wa serikali hapo nje?...

USHAURI wa Daktari Kwa Darassa Baada ya Kupata Ajali ya Gari

Image
  Jumapili Disemba 18 mwanamuziki Darassa akiwa na mtayarishaji wa muziki, Abbah pamoja na mtayarishaji wa video za muziki, Hanscana walipata ajali Kahama mkoani Shinyanga walipokuwa njiani kurejea Dar es Salaam. Katika ajali hiyo ambapo Darassa ndiye alikuwa dereva, wote walinusurika kifo lakini wakiwa na majeraha machache. Baada ya kufika Dar es Salaam, Darassa alikwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajli ya matibabu na baada ya kufanyiwa vipimo, alitakiwa kupumzika kwa muda bila kufanyama matamasha ya muziki au shughuli nyingine ngumu ili aweze kupona majeraha madogo aliyoyapata. Picha: Mwanamuziki Darassa apata ajali Kahama Kupitia CloudsFm leo Darassa amesema kuwa “Nipo hospitalini Muhimbili sasa hivi nawashukuru sana madaktari wa hapa wamenipokea vizuri wamenipa huduma nzuri sana, wamenicheki kwa sababu nilikuwa najisikia vibaya sana sehemu za kichwani nashukuru Mungu majibu yanaonyesha kila kitu kipo poa kabisa kuna damage ndogo wanaifanyia kazi naendelea na mati...

LEMUTUZ Amchana Darasa...Ashangaa Kusikia Anasafari kwa Gari Badala ya Ndege

Image
  lemutuz_nation - LIVE STRAIGHT TALK:- Nilikuwa nasubiri baada ya ajali kwako @darassacmg najua now umepona upo sawa pamoja na kushitushwa na ajali lakini la msingi nimeshitushwa na jinsi ulivyopata ajali please sikutegemea at this stage unapopiga "WIMBO WA TAIFA" bado utaendelea kusafiri kwenye level ambazo hata mimi SOCIAL MEDIA KING nilishazipita that was a shock to me nilidhani huu ni wakati wako wa kusafirina Airbus mpaka Mwanza halafu promoters wanakukodia ndege kutoka Mwanza mpaka Kahama ukiwa na kundi la angalau watu 5 ....please kaa chini jitathmin tena enzi za Show za Vichochoroni zimeisha now it is your time kataa pesa ndogo upate kubwa huwa inaiuma sana kukataa Dola 2,000 but bila kukataa hutapata pesa kubwa na perks kubwa muamuzi ni wewe sio wanaokuzunguka nakuhakikishia kwa Miungu yangu yote wewe sasa ni wa Tsh. 15M mpaka 20M per Show ....halafu management yako inatakiwa kupigana sana kufufua miziki yako ya zamani ambayo haiku hit lakini ni mikali...

MENEJA wa Diamond Aelezea Zilipofikia Collabo za Diamond na Rick Ross na Rihanna

Image
  Hivi karibuni wakati anahojiwa kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, Diamond alitease ujio wa ngoma ambazo amewashikirisha wanamuziki heavyweight wa Marekani, Rick Ross na Rihanna. Jumatano hii kupitia kipindi cha Campus Vibes cha Times FM, meneja wake, Sallam alifafanua zaidi kuhusu hatua iliyofikiwa ya collabo hizo. Sallam alidai kuwa collabo na Rick Ross imeshakalimika, huku ile ya Rihanna ikiwa kwenye hatua za mwisho kwakuwa tayari CV na historia ya Diamond imeshatumwa kwa uongozi wake kuweza kufikiwa maamuzi ya mwisho. Kuhusu nyimbo alizoshirikishwa Diamond, Sallam alisema mwakwani itatoka ngoma aliyoshirikishwa na Burna Boy na Cassper Nyovest huku pia Dj Van wa Morocco akimshirikisha pamoja na msanii mkubwa wa Dubai. Alidai kuwa kutokana na ubusy alionao hitmaker huyo wa Salome, imekuwa ngumu kupata muda wa kushoot video ya wimbo alioshirikishwa na msanii wa Jamaica, Alaine, wimbo alioshirikishwa na msanii wa Ivory Coast Serge Beynaud pamoja na kukamilisha wimbo ...

Niyonzima aongoza mgomo wa mazoezi Yanga

Image
  Kocha wa klabu ya Yanga Mzambia, George Lwandamina, amekumbana na ugumu mkubwa kwenye kazi yake baada ya wachezaji kugomea mazoezi kutokana na kutolipwa mshahara wao wa mwezi Novemba. Nahodha wa Yanga Haruna Niyonzima ameiambia mtandao wa Goal, wameona ni vyema wakagomea kufanya mazoezi ili kuushawishi uongozi waweze kuwalipa mishahara yao ili kuweza kujikimu kimaisha. “Nikweli hii ilikuwa ni makubaliano ya wachezaji wote ndiyo maana jana jioni tulikwenda mazoezini lakini hatukufanya mazoezi na leo kama tulivyofanya leo asubuhi, amesema Niyonzima. Kiongozi huyo wa wachezaji amesema maisha yamekuwa magumu na wao wanategemea mishahara yao ili kuweza kupata huduma mbalimbali hivyo kufanya hivyo wanaamini uongozi wa Yanga utawasikiliza na kulipatia ufumbuzi haraka.  mbele yao ambapo timu yao inakabiliwa na ushindani mkali wa kupigania ubingwa kati yao na wapinzani wao Simba hivyo nivyema wakawaanda kisaikolojia wachezaji ili waweze kupambana katia mechi zao kuliko k...

Timu ambazo zipo juu yetu hazistahili kuwa hapo – Mourinho

Image
  Kocha wa klabu ya soka ya Manchester United, Jose Mourinho amefunguka nakutoa mtazamo wake kwa timu ambazo zipo juu yao zimewazidi pointi. “Ninapoangalia timu nyingi zilizopo juu yetu kwenye msimamo hazistahili kuwa pale kwa sababu kwa kiwango cha kandanda tunazifunika sana!” anasema Jose Mourinho. Manchester United ambao kwasasa wanashika nafasi ya 6 wakiwa na alama 30 katika msamamo wa ligi kuu ya Uingereza huku klabu ya Chelsea ikiwa ndio inaongoza ligi hiyo ikiwa na alama 43.